Friday, May 25, 2012

CANCER 

As we age, there is an increase in the number of possible cancer-causing mutations in our DNA. This makes age an important risk factor for cancer. Several viruses have also been linked to cancer such as: human papillomavirus (a cause of cervical cancer), hepatitis B and C (causes of liver cancer), and Epstein-Barr virus (a cause of some childhood cancers). Human immunodeficiency virus (HIV) - and anything else that suppresses or weakens the immune system - inhibits the body's ability to fight infections and increases the chance of developing cancer.

The following topics will guide us

1. Foods as a cause of cancer
2. Foods in the prevention of Cancer
3. Foods in the treatment of cancer
4. List of specific foods that help prevent cancer
5. Foods that promote cancer
6. Diet for preventing each type of cancer
- cancer of the mouth
-brain cancer
-cancer of throat
-cancer of the esophagus
-stomach cancer
-liver cancer
-lung cancer
-breast cancer
-colon cancer
Etc


 Terminologies:
Cancer- an uncontrolled duplication of cells causing a malignant tumor.
It invades surrounding tissues and may entail metastasis(other tumours of the same type appearing far from the original site) and its natural evolution can lead to death


 Carcinogen-food, substance or other agent that fosters the development of cancer.
The most common carcinogens are tobacco smoke, certain food additives such as nitrites,the substances that form during the cooking of meat, chemical contaminants such as pesticides, some viruses and mold and radiation


 Mutagens- substances that produce mutations or changes in the genetic codeIe DNA. Many of these mutations cause cells to become cancerous, thus mutagens are also carcinogens
Finally Anticarcinogens or cancer protection is foods or substances that neutralize the action of carcinogens and slows or prevents the development of cancer.
Virtually all Anticarcinogens are plant based


Foods as a cause of Cancer:
Factors that cause cancer are;
35% Diet
30% Tobacco
6% Genetic
5% Viral causes
4% Work environment
3%Alcohol
3%Environmental pollution
3%Solar radiation
11% Other
You notice DIET is today's primary cancer causing factor.
We are Eating too much animal based foods which foster cancer, in proportion to plant based foods, which protect against Cancer.
To REDUCE cancer risk, AVOID:
-cured meats(sausages, cured ham, bacon etc) grilled meats and very well done/ over cooked or fried meats
-Excess calories from proteins or fat sources especially animal sources such as meats, whole milk, eggs
-Smoked, pickled, salted or highly spiced foods
-Alcoholic beverages,coffee and tobacco: when combined, they potentate their carcinogenic effect


  2. Foods in the PREVENTION of Cancer
Food that are suitable for humans in aiding in the protection of cancer instead of fostering it are precisely the effects of Fruits, Nuts, Whole grains, Legumes and Vegetable

It requires the increase of;
-Provitamins A, vitamins C and E
-Fibre/Roughage
-Phytochemical elements ie flavonoids, isoflavones, caretonoids....beneficial plant chemicals
All these have been experimented and shown to be Anticarcinogens
They are found exclusively in plant based foods


 3. Foods in the TREATMENT of Cancer
Above ALL foods play a vital role in Cancer prevention. However, even when cancer has been diagnosed, diet continues to be vitally important.

All the anticarcinogenic foods described below, particularly fruit treatments, salads and fresh juices are additional treatment resources that shouldn't be ignored.

There is evidence of their effectiveness in slowing the development of malignant cells demonstrating that their use as a therapeutic tool is well founded.


 4. List of specific foods that help prevent cancer
a) Fruit
Together with veggies, is the most effective anticarcinogenic food.
Scientific research shows a diet abundant in fruits prevents most cancers
All fresh fruits are rich in - Antioxidant vitamins ACE and phtochemicals which are capable of neutralizing carcinogenic substances entering the body
So take in as much as you can of
-Citrus such as lemon, oranges and grapefruit
Their anticarcinogenic capacity is due to the combined effect of Vitamin C, flavonoids, limonoids and pectin
-Plums and apples these protect against Colon cancer
-Pineapples prevent stomach cancers
-grapes the resveratrol they contain, particularly in the skin is anticarcinogenic
-Blackberries and other aggregate fruits such as strawberries, blueberries, cranberries, raspberries and currants are rich in anthocynanins, powerful antioxidants that neutrilize the carcinogenic effect of free radicals
-Guava, Kiwis are great due to their high Vitamin C content


  b) Olive oil
Studies conducted reveal, that when it is substituted for other dietary fats we use, olive oil consumption reduces breast cancer risk.
It's anticarcinogenic effect is due to its richness in antioxidants and mono unsaturated fatty acids among others


 c) Wholegrains
The fibre in whole grains accelerates movement through the bowel.
It also retains and removes carcinogenic substances that may be in the digestive tact, excreting them with the faeces.

Fibre in grains and whole-grain bread prevents stomach and colon cancer by reducing the time that this harmful substances are in contact with the mucosa of the digestive tract.
By preventing absorption of carcinogens, fibre protects against other cancers such as pancreatic and breast cancers.
Grains also contain phytates, which as Anticarcinogens, although they also reduce iron and zinc absorption and therefore a multi mineral supplement to add onto the diet is recommended.
- Rye this is the most effective grain in prevention of colon cancer
-Wheat germ because of its antioxidant action halts the processes of cell degeneration and protects against cancer
-Wheatgrass a sprouted version of the wheat grain is rich in antioxidants and is a potent anticarcinogen


 d) Vegetables
All veggies protect against cancer to a greater or lesser degree.
Their richness in Provitamin A, Vitamin C and antioxidant phytochemicals explain their effect; below are some of the most effective;
- Red beets ie beet roots are high in Anticarcinogens
- Carrots their high concentration of beta carotene ie Provitamin A, other carotenoids and fibre explains its proven anticarcinogenic effect
-Botanical family Solanaceae
The veggies of this family protect against cancer particularly tomatoes contain lycopene very effective in preventing prostate cancers, sweet peppers yellow, green, red, Eggplants
This is due to their richness in beta carotene carotenoids and vitamin c all potent antioxidants
- Botanical family Liliaceae
All the veggies of this family particularly onions and garlic contain flavonoids and sulfur acted essences that protect against cancer because they neutralize carcinogenic substances and inhibit or stop the development of tumor cells.
- Crucifers
The plants of this family contain a variet of sulfur acted phytochemicals whose anticarcinogenic effect has been demonstrated in labs. Their effects persists even after cooking. This include Broccoli, Cabbage, Cauliflower and Radishes.


 e)Yoghurt
In contrast to milk, whose consumption is related to a variety of cancers, yoghurt protects against this disease particularly Breast cancer
It contains active bacterial cultures and lactic acid partially explain this protective effect.
Probiotics are Anticarcinogens and are available through natural yoghurt and pils with strains of good bacteria cultures


 f) Legumes
They protect because of their richness in fibre and phytochemicals such as phytic acid and phytates

- Soy and it's derivatives
This include tofu soy meat and soy milk provide a variety of anticarcinogenic phytochemicals. Most effective is Isoflavones, genistein and daidzein. These are veggie hormones phytoestrogens hat avoid the undesirable effects of estrogen, such as its tendency to promote cancer, particularly breast and prostate.


5. Foods that promote cancer
a) Meat
Numerous studies both experimental and statistical have revealed that meat consumption is a significant risk factor in most types of cancer (brain, lung, stomach, kidney, urinary bladder, uterus, ovarian and prostate, breast among others)
Meats particularly detrimental are redmeats ( beef, lamb, goat, pork) their animal fat has been associated with many cancers
Salted/cured meats such as bacon, ham and sausages etc contain nitrosamines which is carcinogenic
Meat cooked well done or grilled on a barbecue or fried cause the formation of heterocyclic amines, aromatic hydrocarbons and benzopyrene which are carcinogens
Hormones used to fatten livestock, when they are present in meat in elevated amounts can be carcinogenic
So eliminate meat from your diet gradually to get off risk of cancers



b) Alcoholic beverages
They promote cancer even when considered to have medicinal value such as wine and beer
These do not require large doses to induce cancer.
This effect is present even with moderate consumption.
Breast cancer risk is increased with an intake of 1 glass a day by 250%
There is proven relationship between overall consumption of alcoholic beverages and cancers of the mouth, throat, breast, lung, liver, pancrease, colon, and urinary bladder


 c) Refined products
When white bread, rolls and other refined products are used in place of whole grains in the diet, there is a corresponding relation to the formation of cancer.
This is y;
- first it lacks fibre
-excess sugar content
-transfatty acids this type of fatty acidosis common in refined industrial baked goods
Fried foods and margarine also contain trans fatty acids
In addition to raising cholesterol levels and promoting heart attack and cardiovascular diseases, they are related to cancers of the breast and skin


 d) Sugar
Some studies have related excess white sugar use with the following types of cancer;
Colon, stomach and cervical
Brown sugar or maple syrup are not as harmful since they contain some minerals and vitamins that refine white sugar lacks
Fructose protects against prostate cancer


 e) Coffee
Coffee consumption has been associated with of the urinary bladder and disease of the breast which can be pre-cancerous
This effect is not due to the caffeine but rather the components of its essence.


 f) Milk
According to various studies excess whole milk consumption is associated with the appearance of some cancers like breast, lung, ovarian, prostate and urinary bladder
Possible explanation is that milk can transmit bovine leukemia virus which is carcinogenic


 g)Eggs
There is evidence that excess consumption of more than 3 eggs a week is associated with cancer of stomach, breast, lung, pancrease, colon, ovaries
Explanation is;
-Cholesterol eggs elevate cholesterol and may promote cancer
-Saturated fat this is predominant fat in eggs which is a factor in cancer development
-Viruses hence the contamination with leukemia type viruses which pass to eggs and cause a variety of cancers
Eggs should be well cooked to prevent infections from salmonella bacteria


 h) Shellfish/ fish
Due to the nature of shellfish living at the bottom of the sea or water bodies, they may contain carcinogenic substances such as lead and mercury dumped into the sea
For other Fish avoid the salted or cured variety as they contain nitrosamines which are carcinogenic


 6. Finally Diets for preventing certain types of cancers
a) Cervical cancer
Increase
Fruits
Veggies especially those high n carotenes such as carrots beet roots
Vitamin C
Folates is B vitamins
Antioxidants Vitamins A,C,E
I advise onto your diet to get a supplement called A Beta Care contains a variety of antioxidants mentioned it retails at 2,800/-
Reduce
Meat
Animal fat
Sugar


b) Ovarian cancer
Increase
Vegetables particularly carrots and beets
Crucifer outs veggies
Whole grain bread and pasta
Fish
A Beta Care
Reduce
Meats
Whole milk
Saturated fats
Eggs
Butter


) Prostate Cancer
Increase
Fruits
Vegetables
Lots of tomatoes
Wholegrains cereals, breads and pasta
Legumes - soy
Garlic and onions
Beta carotene
A Beta Care
Pro 6 retails for 3,000/-
Reduce or eliminate
Red meat and cured/salted/smoked meats n fish
Eggs
Animal fats
Margarine
Cholesterol bad ones which are HDLP


d) Colon cancer
Increase
Fibre
Fruit
Veggie carrots spinach wheatgrass and beets especially
Whole grain breads and pasta
Fermented dairy products yoghurt
Calcium as a food supplement retails 2,400
Reduce or Eliminate
Reduce meats ( beef, pork, lamb)
Well done meat
Processed or cured meats
Liver and other variety meats
Eggs particularly for women
Fats and high calorie foods especially animal based
Cured high-fat cheese
Sugar such as is added in coffee or tea
Alcoholic beverages


   e) Breast Cancer
Increase
Soy, tofu, soy milk
Fruits
Vegetables ESP spinach, wheatgrass, carrots, broccoli
Olive oil
Garlic/ onions
Yoghurt
Fibre
Vit ACE
Beta carotenes
A Beta Care
Arctic Sea has olive oil 2,900
Reduce orEliminate
Red meat ( fish and skinless chicken are not detrimental)
Processed pork sausages, bacon, ham
Eggs
Fat animal sources
High fat cheese
Trans fatty acids found in margarine and commercial baked products
Alcoholic beverages even in low doses
Chocolate and pastries


 f) stomach cancer
Increase
Fruits particularly citrus and pineapple
Vegetables
Garlic and onion
Whole grain bread
Vegetable oil
Whole grain pasta and rice
Wheatgrass
Arctic sea
Aloe Vera
Reduce or eliminate
Red meat ESP well done
Cured meats and sausages ESP homemade
Beer
Salt cured foods
Eggs
Rolls and pastries
Sugar
Saturated fats


 g) Lung Cancer
Increase
Fruits and vegetables
Wheatgrass
A Beta Care
Arctic Sea with olive oil
Reduce or Eliminate
Cured meats sausage bacon
Beef
Whole milk and diary products
Eggs
Refined baked products


 h) Brain Cancers
Increase
vitamin E
A beta Care
Arctic Sea
Wheatgrass
Reduce or eliminate
Hot dogs intake by pregnant women can increase risk of cancer to unborn
Hamburgers
Cured or roasted meats
Processed pork products such as boiled ham and bacon
Fried foods

 
I) Liver Cancer
Increase
Vegetables
Vitamin ACE
A Beta Care
Wheatgrass
Reduce or eliminate
Pork
Wine
Moldy foods or those with aflatoxin residue
Alcoholic beverages
Beers



Tuesday, May 15, 2012

Rotavirus disease

  • Rota virus is the most common cause of severe diarrheal disease in children worldwide and is responsible for the deaths of more than 450,000 children each year, 85 percent of whom live in developing countries.
  • Rota virus accounts for 37 percent of global child deaths attributable to diarrhea and 5 percent of all deaths in children younger than age five.
  • Rota virus is found in all countries. Regardless of hygiene practices or access to clean water, nearly every child in the world will be infected with rota virus before age five.
  • In young children, rotavirus disease is characterized by diarrhea, vomiting, fever, and severe dehydration. In fatal cases, death is caused by severe dehydration due to rota virus infection.
  • Rota virus disease cannot be treated with antibiotics or other drugs. Re hydration therapy is an important part of treating dehydration due to diarrheal diseases, including rota virus. Vaccination offers the best hope for preventing severe rota virus illness, particularly in settings where access to medical care is limited.

Rota virus vaccines

  • There are two currently licensed vaccines against rota virus: Merck’s RotaTeq® and GlaxoSmithKline’s Rotarix®. Studies of these vaccines have demonstrated their safety and efficacy among children in every region of the world. Safety and efficacy trials in Africa and Asia found that the vaccines dramatically reduced severe disease among infants in developing countries, where the majority of rota virus deaths occur. Results from these trials are essential to national governments as they make informed decisions about introducing rota virus vaccines into the public sector.
  • In 2009, the World Health Organization recommended that rota virus vaccines be included in every country’s immunization program.
  • Where they have been introduced, rota virus vaccines are making a major impact—slashing hospitalizations due to rota virus, while also reducing hospitalizations for diarrhea of any cause. Rota virus is less prevalent among unvaccinated children, as well, suggesting herd immunity as an indirect result of rota virus vaccine introduction.
  • While current manufacturers play an important role in meeting the global demand for the existing vaccines, additional vaccine options and manufacturers are critical to ensuring a sustainable, affordable supply. Several manufacturers are developing rota virus vaccines, including many from developing countries.
  •   Rota virusvaccines are an important part of an integrated prevention and treatment strategy to control diarrheal disease. Other elements of this strategy include low-osmolarity oral re hydration solution; zinc supplementation, exclusive breastfeeding, proper nutrition, and safe water.

Related diseases

Diarrheal disease is the second leading cause of death in children in developing countries and the most common cause of childhood deaths in Africa. In addition to rota virus, there are many pathogens that contribute to morbidity and mortality from diarrheal disease, including Shigella and enterotoxigenic Escherichia coli (ETEC), the leading bacterial causes.

Where in Tanzania can we get Rotavirus vaccine?

In Tanzania, local government hospitals do not have this vaccine as it is termed as "EXPENSIVE". Hence the only hospitals that give this vaccine are private hospitals which according to sources are only two namely The Trauma Center and Premier Care Clinic located in Dar es Salaam Tanzania. However, these are the only private hospitals that provide this vaccine.


What is the Cost of the Vaccine?


At The Trauma Centre the vaccine is USD 75 and at Premier Care clinic it is TZS 120,000.

AWARENESS

The Rota virus Vaccine can only be given to a baby between 0-4months. Above this age bracket a child cannot be vaccinated. A professional doctor source says this is because Rota virus in children of the age bracket 0-4months is more severe than in older children. Though parents are advised to keep the children hydrated by either giving them lots of fluids n juice and ORS (Oral Re hydration Salts) come in handy when a child is infected by Rota virus. ORS consists of a solution of salts and sugars that is taken by mouth.

Mamaz lets be on the front line to make sure that our children get the best in so doing we will save our children's lives. No matter how expensive these vaccines are our children are priceless n they are the leaders of tomorrow so lets do our best to save their lives by vaccinating them!!



Friday, April 27, 2012

UFUGAJI WA KUKU


Kuna usemi flani unatumiwa na watu wengi sana. unasema; “kazi ndio msingi wa maendeleo ya mtu yeyote” . Hata mimi nakubaliana na usemi huu kwani ni kweli kabisa kazi ndio msingi wa hatua yoyote ya maendeleo ya mtu yeyote chini ya msingi mkuu ambao ni Mungu. Kinyume chake, asiyefanya kazi (ya kuajiriwa/kujiajiri) basi atabaki kuwa maskini na mtu wa shida ya kipato, mahusiano mabaya na wanadamu wenzako, kuwa tegemezi nk. Kwa kuwa tunatamani sana kutoka katika kongwa hili la umasikini wa kipato na hali mbaya ya maisha, tunalazimika kufanya jukumu letu kuu la kumuomba sana Mungu ili atuwezeshe kujua na kufahamu mbinu mbalimbali kisha kujifunza na kufahamu kwa makini tena kwa njia rahisi mno za kututoa katika hali hii ya umaskini uliokithiri.

Ikumbukwe kwamba, kujifunza kwa msisimko tu bila ya kuyaingiza mambo hayo uliyojifunza katika mazoezi na vitendo vya makusudi maishani mwetu ni wazi kwamba hayatatusaidia, bali yatabaki vichwani mwetu kama hadithi tu za alfulelaulela na maisha ya kubahatisha maarufu kama akadabraakadabra. Hivyo tumuombe sana Mungu wetu ili mafundisho haya yaweze kubadili maisha yetu kwa uchumi bora na endelevu ili tuweze kupata kipato na kurudishia Mungu zaka na sadaka badala ya kukaa kulalamika kuwa hatuna cha mkurudishia muumba wetu YEHOVA.
Kama ilivyo chunvi ya dunia, ufugaji pia huhitaji upendo, uvumilivu, karama, utu na maombi ya dhati ambayo yatazaa namna nzuri ya kuipenda kwa dhati ya moyo wako kazi hii ya ufugaji. Vinginevyo utabakia kuwa mtu wa kujaribu na kuishia kushindwa kila mara. Kama ilivyo kanuni ya maendeleo yoyote yale, ufugaji wa kuku pia huhitaji; Ubunifu, utundu wa akili, kujaribu bila kukata tamaa, kugundua, kujifunza, kufanyia kazi mawazo yaa wengine, kusoma vitabu na majarida mbalimbali yahusuyo kazi yako, kujishughulisha nk. Hata ukifundishwa darasani huwezi kufundishwa vyote na mwalimu wako, vingine itakubidi utafute mahali pengine kwa ubunifu mkubwa, ugunduzi na mambo mengine mengi ili ufanikishe lengo la kupata elimu bora ya kile unachokitaka. Hii huhusisha akili yako vema katika kujifunza kutoka kwa watu au vitu vingine nk. Lakini mafanikio zaidi yatapatikana pale utakapokuwa katika utendaji zaidi.


UFUGAJI WA KUKU WATANO (5) WA KIENYEJI UPATE KUKU MIA MBILI (200) KWA MIEZI SITA (6) TU!
(Kuku 200 x 5,000 = 1,000,000)

Unaweza ukaniona kama mimi ni kichaa na ninaye ota ndoto za mchana ambazo hazina mafanikio wala tija maana nadharia hii inaweza isiwaingie vizuri watu vichwani mwao. Watu wengi wamekuwa wakisema na kushauri hata kushauriwa hata na wale wasiofaa. Ninaamini wengi wetu hawapendi kuamini kile wanachoambiwa hadi pale watakapoona kwa macho yao ndipo waamini (akina Tomaso). Sikia nikuambie! kama huamini haraka kitu chochote hebu usimkatishe tamaa yule aliyekwambia habari hizo za kukatisha tamaa, badala yake jaribu kupeleleza na kufuatatilia hatua kwa hatua tena kwa makini maelezo uliyopewa, kisha yaweke katika utendaji (tenda/fanya) kwa ufanisi kisha subiri matokeo. Baada ya kupata matokeo sasa unaweza kwenda mbele kidogo ukauliza/kusoma/kujifunza zaidi ili kuona kama kuna mahali umekosea au hukuzingatia kanuni na maelekezo uliyopewa. Baada ya kupata maelezo ya ziada hebu rudia kufanya tena kwa kuboresha kupitia maelekezo ya awali na hayo mapya uliyopata yote kwa pamoja ili upime matokeo yake. Hapo sasa utakuwa upo kwenye haki ya kuamini au kutoamini kwamba jambo hilo ni kweli au siyo kweli na siyo kutaa tu kwa ubishi usiokuwa na maana yeyote. Kwa kufanya hivi hakika utapiga hatua mbele katika kuboresha maisha yako ya sasa na ya baadae. Ila ukifanikiwa usije ukamkufuru Mungu aliyekuwezesha.
Hebu anza na kuku Watano (5) tu Majike wenye Rika/Umri mmoja (au wanaokaribiana). Watunze vizuri kwa kuwapatia chakula kilicho na mchanganyiko kamili wa viini lishe vinavyotakiwa katika mwili wa kuku, yaani; wanga, protini, calcium, chumvichumvi, madini joto nk (kama nilivyoeleza hapa chini). Wawekee na Jogoo mmoja mzuri wa kienyeji/kizungu/chotara (kama nilivyoeleza hapa chini juu ya uchaguzi wa majogoo).

Wanapoanza kutaga watayarishie mahali pazuri/Kiota kizuri cha kutagia na kuatamia kwa kuwajengea viota ndani ya banda. Hakikisha mahali hapo hapavuji wala hapapati unyevunyevu wala joto kali sana. Hakikisha mahali hapo pana usalama wa kutosha (mahali wanyama hatari kama vicheche, pakashume, nyoka nk hawawezi kufika).

Kuku wakiendelea kutaga na sasa ukaona wanakaribia kuatamia,Anza kuchagua aina ya mayai unayotaka kuku wako walalie. Hii inamaanisha kuwa; ukichagua mayai makubwamakubwa hayo yanakuwa na vifaranga majogoo na mayai madogomadogo mara nyingi huwa ni ya vifaranga majike. Acha kuwawekea mayai ya mviringo kama mpira!

Hakikisha kuku wote wanasubiriana ili walalie/waatamie kwa pamoja.

Weka mayai 12 hadi 15 kwa kila kiota cha kuku 1 kulingana na umbo la kuku wako. Kuku anaweza kutaga hadi mayai 30 kwa kila msimu wa kutaga unapofika. Unaweza kutumia mayai machache kati ya 30 kwa kumuatamishia kuku wako huku mayai mengine yakisubiri awamu ya pili ya kuatamiwa.Kwa mfano ukiwawekea kuku wako hao watano, Kuku 5 x Mayai 12 = Mayai 60.

Kwa kawaida kuku huatamia/hulalia mayai kwa siku 19 hadi 21/24 tu hadi anapototoa vifaranga. Hakikisha unawawekea kuku walioatamia chakula chenye viini lishe vya kutosha na maji mengi karibu na viota vyao ili wakitoka kwenye viota vyao wale chakula mara moja na kunywa maji kisha warudi haraka kwenye mayai yao. Hii itasaidia kuangua mayai yote 12/15 bila kuharibu yai hata moja. Au hata yakiharikbika basi hayataharibika mengi kama ukiacha kuwawekea chakula waende kufukuzana na panzi na vyakula majalalani huko nje na kuchelewa kurudi kwenye mayai yao.

Wakati ukisubiria siku hizo 21/24 anza kujenga kibanda kidogo ndani ya banda kubwa ulilojenga awali au jikoni au andaa boksi kubwa na gumu kwaajili ya kutunzia vifaranga watakaoanguliwa ndani ya siku 21/24 zijazo.
Baada ya kuku hao 5 kuangua vifaranga wako 60 hapo ndipo kazi kubwa ya kulea vifaranga inapoanza. Elewa kuwa ili upate mafanikio haraka hakikisha kuwa kazi ya kulea vifaranga inakuwa yako na siyo ya kuku! Kwanza, Unatakiwa kuondoa na kuchoma moto/kufukia mabaki yote ya mayai na kuboresha usafi wa banda lote ili kuepusha magonjwa kama vile kuharisha, viroboto, papasi nk. Hapo unaweza kuwatoa vifaranga wako wote 60 mmojammoja kadri wanavyoanguliwa hadi kufikia kifaranga wa mwisho, yaani Yule wa 60 na kuwaweka katika kibanda kidogo/boksi ulichokijenga na kuwawekea mayai mengine mama zao (yale 15/18 kati ya 30 uliyoyabakiza) ili waatamie tena kwa siku 21 hadi 24 zingine. Unapotoa kifaranga kutoka kwa kuku aliyeatamia humfanya kuku Yule ashindwe kutoka kwenye mayai maana hana mtoto wa kulea.

Akimaliza kuangua mayai yote na ukamuwekea mengine ni rahisi kwake kuendelea kuatamia maana atasubiri kupata vifaranga na ndipo atajikuta amelalia kwa siku 21 zingine bila wasiwasi. Kwa kufanya hivyo utakuwa tayari umejipatia vifaranga/kuku zaidi ya 100 ndani ya wiki 7 tu! Sasa Unatakiwa kuwajali sana kuku hawa wanaolalia kwa mara ya pili kwa kuwapa chakula cha kutosha, maji, majani ya makongwe, mchicha, mchunga nk ili wapate vitamini na madini mengine muhimu kwa afya zao. Fanya hivyo hata watakapokuwa wametotoa na ukawanyang’anya vifaranga. Hii itawasaidia ili wasinyonyoke sana manyoya maana kuku wengi hunyonyoka manyoya wanapoatamia. Kwa kufanya hivi, kuku wako watakaa kwa wiki 2 hadi 3 bila vifaranga na kisha wataanza kutaga tena na kuatamia kama mwanzo.

Vifaranga
wako hakikisha unawatengenezea chumba chao kido ndani ya banda kubwa/jikoni, kisha wawekee chanzo chochote cha joto kama vile; taa ya chemli/jiko la mkaa/vizinga vya moto nk ili wasiathiriwe na baridi hasa wakati wa usiku. Umakini mkubwa sana unatakiwa hapa! Hakikisha unakuwa makini wakati wa usiku ili kuongeza na kupunguza joto ndani ya kibanda cha vifaranga maana wakati huu maranyingi joto hupungua na ubaridi huongezeka na hivyo unaweza kuua vifaranga wako.

NAMNA YA KULEA VIFARANGA.
Katika ulezi wa vifaranga kama kuku utawanyang’anya vifaranga vyao utatakiwa kuwajengea banda dogo (ndani ya banda kubwa/uzio) ili uwawekee chanzo cha joto kama taa/jiko la mkaa (kama ni sehemu/majira ya baridi). Kama utatumia jiko la mkaa unatakiwa kuacha kwanza hadi mkaa mweusi uwake wote ndipo uweke bandani maana mkaa ukitoa moshi unaweza kuathiri vifaranga vyako. Angalia namna ya kuweka jiko lako la mkaa juu kidogo ili vifaranga wasiungue. Hakikisha taa yako haitoi moshi sana na haivujishi mafuta. Pia uwe na akiba ya mafuta ya taa ya kutosha. Usiweke mafuta mengi kwenye taa maana inaweza kulipuka ikakuletea hasara. Vifaranga wasizidi 50 kwa boksi 1. Hakikisha umewasha taa/jiko lako ndani ya boksi saa tatu au zaidi kabla ya kuwaweka vifaranga ili chumba/boksi lipate joto kabla ya vifaranga kuwasili. Njia hizi zinahitaji uangalifu wa hali ya juu sana kwani kuhatarisha/kuua vifaranga ni kuhatarisha maendeleo yako. Kama utaamua kutumia umeme pia ni vizuri zaidi maana inapunguza hatari zaidi.

Kwa hiyoa njia zote tatu unaweza kutumia jedwali lifuatalo ili kuweza kumeneji joto la kibanda cha vifaranga;
UMRI WA KKUKU/VIFARANGA
JOTO NDANI YA BOX/KIBANDA CHA KULELEA VIFARANGA
JOTO NDANI YA CHUMBA/BANDA
Wiki 1
33-35oc
30-32oc
Wiki 2
30-33oc
27-29oc
Wiki 3
27-31c
24-26oc
Wiki 4
24-29oc
21-23oc
Wiki 5
26-27oc
22-23oc

Baada ya wiki ya 4/5 pasua box/watoe kwenye banda la kulelea ili walelewe kwa joto la kawaida la banda/chumba.
Kwa kawaida joto hupimwa kwa kipimajoto (thermometer), lakini kama huna kipimo hiki, njia rahisi ni kuwaangalia kulingana na tabia zifuatazo; Kama vifaranga wamejikusanya sehemu moja basi joto ni kidogo bandani mwao, au kama wanaenda mbali na chanzo cha joto huku wanatanua mabawa yao na wakihema harakaharaka basi joto ni kali/limezidi kiwango. Pale watakapo tawanyika vizuri ndani ya boksi/kibanda cha kulelea huku wanakula na kunywa maji vizuri basi joto ni la wasta na ndilo linalofaa. Kama unatumia njia ya Boksi, basi unatikiwa kulipanua kulingana na ukuaji na mahitaji ya vifaranga vyako.
Vifaranga wako wape chakula cha vifaranga cha kutosha, maji safi na salama, majani mabichi ambayo hufungwa kwa kuning’inizwa kwa kamba,na CHANJO za minyoo nk ili wapate vitamin, madini na protini itakiwayo na kuzuia tabia ya kudonoana ili wakue vizuri.
Hakikisha kuwa chumba chao ni kisafi na hakina unyevunyevu wakati wote. Unyevunyevu husababisha ugonjwa wa baridi na hufanya vifaranga wajikunyate na kutetemeka na wanaweza kufa ghafla!
Inashauriwa kuwa siyo salama kufuga aina nyingine ya ndege kama vile njiwa, bata, bata mzinga nk kwa kuwachanganya na kuku maana kila aina ya ndege wanamagonjwa yao. Hivyo kuwachanganya kutakufanya ushindwe namna ya kuwatibu wanapopatwa na ugonjwa. Pia chawa wa njiwa huleta ugonjwa wa Ndui hasa kuku wanapoangua vifaranga wao. Hapa ugonjwa unaweza kufyeka vifaranga wako wote 60/100 kama utafuata ushauri wangu!
Baada ya wiki 2 hadi 3 baada ya kuwanyang’anya vifaranga kuku wako wataanza tena kutaga mayai. Wakiatamia wote 5 Kama utaimarisha huduma kwao na kwa vifaranga/kuku wale 100 tayari utakuwa una kuku 105 au zaidi. Kuku wale 5 wa mwanzo wakiatamia tena kwa siku 21 hadi 48 (kama utafuata mfumo ule wa mwanzo wa kuaatamishia mara 2) utajipatia vifaranga wengine 100 tena na hivyo kuwa na kuku zaidi ya 200 ndani ya miezi 5/6 tu! Ukiwahudumia vifaranga wale wa mwanzo 100 vizuri kwa miezi 3 na nusu nao wataanza kutaga kama mama zao. kwahiyo, Chukulia walalie majike 5 wa mwanzo na majike 50 waliopatikana baada ya uzao wa kwanza kwa miezi ile 3 ya mwanzo utakuwa na mitetea 55. Wote wakiatamia na watoe vifaranga 10 kila mmoja kwa siku zilezile 21 hadi 46, tayari utakuwa na vifaranga 550! Sasa jumlisha na wale 150 waliobakia kati ya kuku 200 na wote wakakua vizuri utapata kuku na vifaranga zaidi ya 700! Jumlisha na 550 watakaototolewa na mama zao wale 5 wa

kwanza na wale 50 wa uzao wa 1 na 2 kwa mara ya 2 si tayari utakuwa na kuku zaidi ya 1,200 ndani ya miezi 6 hadi 8 tu? Hivyo utajikuta unao kuku zaidi ya 1,000!
Kati ya kuku 1,000 ukisema utoe kuku 800 wa kuuza na ukiwauza kwa bei ya Tsh. 4,000 kwa kila kuku 1 tayari utakuwa na Jumla ya Tsh. 3,200,000/= ambazo unaweza kufanya mtaji wa mambo mengine au kuboresha mradi wako zaidi. Unafikiri hapo hujaanza kufikia lengo la kuku 1 akuletee shilingi Milioni 1? Ukiendelea hivi inamaana kuku 1 atakuzalishia zaidi ya hapo.

BANDA LA KUKU.
Unatakiwa kuwa na banda bora la kufugia kuku ambalo litaweza kutunza kuku ili wasiweze kupatwa na madhara mbalimbali kama vile; kuliwa/kujeruhiwa na wanyama wakali, kuchukuliwa na wezi nk. Lakini banda bora pia litawasaidia kuku kuhimili mabadiliko mbalimbali ya hali ya hewa yanayoweza kujitokeza.
Sehemu ambayo inafaa kwa ujenzi wa banda bora ni ile ambayo inaweza kufikika kwa urahisi, iwe na mwanga wa kutosha, isiwe na upepo mkali na isiyoruhusu maji kusimama au kuingia ndani.
Banda ni vema likawa la ukuta/mbao/mabanzi.matete/mianzi imara ili lishikilie paa vizuri lisianguke. Kuta hizi zaweza kujengwa kwa matofali ya saruji/matope/kuchomwa/mabanzi/mbao nk. Katika kuezeka waweza kutumia mabati/vigae/nyasi. Banda ni vema likawa kubwa kulingana na kiasi cha kuku na umri walionao. Kitu cha kuzingatia ni kwamba banda liwe na hewa ya kutosha.
Kuku wanaofugwa ndani ni vema wakatengenezewa uzio mpana (angalau Mita 8x10) ili wapate mahali wanapoweza kuota jua, kupumzikia/kupunga hewa na kufanya mazoezi (wawekee kamba/bembea/ngazi ndani ya banda). Hakikisha kuwa banda ni imara na hawatoki nje ya banda na kwenda mbali ili uweze kuwawekea chakula cha kutosha na maji na hata wale wanaotaga/kuatamia wapate chakula na kurudi haraka.
Banda likiwa kubwa na bora litapunguza magonjwa kwani litakuwa na hewa ya kutosha ambayo itasaidia kupunguza joto na unyevunyevu usio wa lazima bandani mwako. Hii itasaidia uingizaji oksijeni ya kutosha na kupunguza hewa chafu zenye madhara kwa kuku. Pia litasaidia namna ya kufanya usafi kwa urahisi na kupunguza vumbi ambalo linaweza kusababisha kikohozi kwa kuku wako. Ni vema banda lisipungue Mita 3 kwenda juu.

Mambo muhimu ndani ya Banda.
1.       Mambo muhimu ndani ya Banda.
1.  Sakafu nzuri (iliyotengenezwa kwa saruji/udongo ili isituamishe maji. Isiwe na nyufa ili iweze kusafishwa kwa urahisi.
2.  Hakikisha kuwa banda linakuwa na Viota (vitagio) vizuri kwaajili ya kutagia. Viota viwe na urefu wa Sentimita 30 na upana sentimita 30 na kina sentimita 35. Sehemu ya mbele izibwe kwa sentimita 10 tu chini. Sehemu zote hizo zizibwe kwa ubao. Kama kuku wako ni wakubwa unaweza kuongeza upana, urefu na kina kiasi cha kutosha mfano, Upana na Urefu 35cm, kina 55cm nk. Hakikisha kiota/kitagio kinakuwa na giza kiasi maana kuku hupenda kutaga mahala pa giza kidogo/palipojificha. Giza litasaidia kuku asiweze kula mayai au asiweze kudonoana na kuku wengine. Kiota pia kinatakiwa kiwe mahali ambapo ni rahisi kwa kuku kuingia na kutoka, pia iwe ni rahisi kusafisa.
Ndani ya kiota kuwekwe majani makavu/maranda ya mbao laini na kinyunyize dawa ya unga ya kuzuia viroboto/utitiri kabla ya kuweka nyasi.
AIDHA, ni vizuri sana kuwawekea kuku wanaoatamia mayai wakati wa usiku maana ukimuwekea wakati wa mchana anaweza kuyaacha.
Kuku anayetarajiwa kuatamia ni vema akachunguzwa kama anao utitiri/viroboto/chawa kwenye manyoya yake. Wadudu hawa humkosesha raha kuku anayeatamia na wengi huacha mayai na kukimbia/wasitulie kwenye viota vyao. Hali inapelekea kuanguliwa kwa vifaranga wachache. Unaweza kumuona mtaalam wa mifugo kwa ushauri zaidi.
1.  Banda liwe na vichanja maana kuku hupenda kulala juu ya vichanja maana nao ni ndege.
2.  Vyombo safi na vizuri kwaajili ya chakula na maji.
3.  Walazie majani makavu/maranda ya mbao/makapi ya mazao sakafuni kwa banda zima.
UCHAGUZI NA UHIFADHI WA MAYAI.
Mayai huharibika kwa urahisi sana yasipo tayarishwa na kutunzwa vizuri kwa uangalifu. Matayarisho huanzia bandani hadi ndani kwa kufanya yafuatayo;
o   Hakikisha viota vyote ni safi wakati wote.
o   Chakula kiwe ni cha kuimarisha gamba la yai na vyakula vingine.
o   Vyombo vya kukusanyia mayai viewe safi na imara.
o   Kusanya mayai mara2 hadi 3 kwa siku ili kuepuka mayai kuvunjwa/kuliwa/kuchafuka kwa mayai mengi na kupoa haraka.
o   Ondoa mayai yaliyo na nyufa na maganda yasiyo imara.
o   Safisha mayai mara baada ya kukusanya na kabla ya kuweka kwenye chombo cha kuhifadhia saa 12-24. Mayai yanaweza kuoshwa kwa maji ya uvuguvugu (nyuzijoto 35oc) na kusugua taratibu kwa mkono ili kuondoa uchafu (kama upo). Lakini unashauriwa kusugua kwa mkono bila maji ili kusafisha maana maji hupunguza ubora wa yai na maranyingi yai huharibika haraka.
o   Weka katika vyombo visafi kwa kuelekeza sehemu ya yai iliyo pana iwe juu na sehemu nyembamba iwe chini, beba kwa uangalifu.
o   Hifadhi mayai katika sehemu ya baridi nyuzijoto10 hadi 16 za sentigredi.
o   Mayai yapangwe kwa daraja kwa kufuata ukubwa na rangi ili kuvutia wateja na kuongeza bei. Pia unaweza kuweka kwa kufuata muda unapoyaokota kutoka bandani. Weka lebo yenye tarehe ili usichanganye wakati wa kuwaatamishia kuku wako/kuuza.



Kuchagua mayai ya kuatamishia kuku kwaajili ya kuangua vifaranga.
Mayai yanayofaa kwa kuatamiwa na kuanguliwa ni vema yawe na ukubwa wa wastani, yasiwe na ufa/nyufa, yasiwe ya mviringo kama mpira, yasiwe na uchafu wowote juu ya gamba lake, yasiwe yametengwa kwa zaidi ya wiki 1 (siku 7).
1.       NJIA MBALIMBALI ZA UFUGAJI WA KUKU.
Kuna njia kuu mbili za ufugaji wa kuku.
1.  Ufugaji Huria
Aina hii ya ufugaji, kuku huachiwa huru wajitafutie chakula na maji wao wenyewe. Utaratibu huu hutumika zaidi kufugia kuku wa kienyeji ambapo mfugaji hupata hasara na pengine hupata faida kidogo maana kuku hukosa uangalizi na hawapewi chakula cha ziada.
Faida.
o   Haina gharama kubwa za ufugaji.
o   Kuku hupata mazoezi ya kutosha.
Hasara.
o   Huharibu mazingira maana hula nafaka, mazao nk.
o   Ni rahisi kuambukizwa na kusambaza magonjwa.
o   Ni rahisi kuathiriwa na hali mbaya ya hewa, watu na wanyama wakali kama paka, vicheche, mwewe, kipanga, nyoka nk.
o   Ni rahisi kutaga mayai porini/vichakani na hivyo mayai/kuku mwenyewe kupotea.
o   Ukuaji wake ni hafifu/uliodhorota.
o   Kuna uwezekano wa kuhamia nyumba nyingine/kwa jirani kwa urahisi.
1.  Ufugaji wa ndani ya Uzio/Banda.
Hufanyika katika sehemu iliyozungushiwa uzio/ndani ya uzio maalum ambapo kunakuwa kuna utaratibu wa kuku kupewa chakula na maji kwa urahisi. Ndani ya uzio huwekwa banda zuri, bora na imara ambalo huruhusu kuku kuingia na kutoka wanapopumzika/kulala/kutaga mayai. Ufugaji huu hutumika zaidi kwa kuku wa kigeni na kuku chotara na hata wa kienyeji pia.
Faida.
o   Gharama ya ufugaji wake ni kubwa.
o   Faida yake ni kubwa hasa ukufuga kibiashara.
o   Ni rahisi kuelewa kiwango cha utagaji na utotoaji wa kuku wako.
o   Ni rahisi kufahamu kuku wazuri wa kuatamiashia mayai na kulea kwa faida ya haraka.
o   Siyo rahisi kuku kuathiriwa na wezi/wanyama/vicheche/mwewe/hali mbaya ya hewa.
o   Siyo rahisi kuambukizwa magonjwa mbalimbali kutoka nje.
o   Ni rahisi kutibu na kujua maendeleo ya kuku wako kwa urahisi.
o   Wanakuwa na usalama wa uhakika.
o   Faida zake ni nyingi kuliko ufugaji huria.
Hasara
o   Gharama za mwanzo za ujenzi wa banda, uzio na vifaa vya chakula na maji ni kubwa kiasi. Hivyo zinahitaji mtaji.
o   Njia hii inahitaji eneo kubwa na huru.
o   Ni rahisi kuambukizana ugonjwa kama itatokea.
o   Ufugaji huu unahitaji utaalam na umakini wa kutosha

1.       UCHAGUZI WA KUKU.
Chagua kuku wenye sifa zifuatazo;
o   Wenye kukua haraka,
o   Wenye uwezo wa kustahimili magonjwa,
o   Wanaotaga mayai mengi,
o   Wawe na uwezo wa kuatamia na kuangua vifaranga wengi na kuwalea (jike/mtetea).


Ni vema sana kutumia majogoo chotara au majogoo wa kienyeji wale wakubwa, warefu, wenye kucha fupi. Chagua wenye maumbile mazuri, uzito wa wastani na wawe wenye rangi za kuvutia kisha uwachanganye na majike/mitetea yenye umbo zuri, uzito mzuri na rangi nzuri ili kupata kuku chotara wanaokua haraka na wenye uzito mzuri kwaajili ya biashara nk. Kama huna kuku wenye sifa hizo basi ni bora sana ukanunua kutoka mahali pengine.
Wakati wa kuatamia ni vema kuku mmoja apewe/awekewe mayai 12 hadi 15 kwenye kiota chake mwenyewe na siyo kuwachanganya kama wakati wa kutaga maayai. Kama wametotoa kuku 2 au zaidi kwa wakati mmoja ni vema aangaliwe kuku mwenye uwezo wa kulea vifaranga ili aachiwe vifaranga vyote (kama utashindwa kuwatengenezea boksi/kibanda cha vifaranga kama nilivyoshauri hapo juu) na kuku wengine watengwe na vifaranga ili waanze kulishwa vizuri na kuchanganywa na majogoo, hapa wataanza kutaga baada ya wiki 2 hivi.




MUHIMU: Ni vema sana kutofautisha makundi ya kuku kulingana na umri wao ili kupunguza kuku kudonoana/kuumizana.
1.       NAMNA BORA YAKULISHA NA KUNYWESHA KUKU.
1.  MAJI.
Maji ni muhimu sana kwa kuku wawapo bandani. Wape maji ya kutosha kila wakati unapoona yanapungua/kuisha ili waendelee kuyeyusha chakula wanachokula Nna kupunguza joto mwilini. Kuku 1 anaweza kunywa hadi robo lita ya maji kwa siku. Kwa hiyo utawawekea kulingana na wingi wao. Pata chombo kizuri ili uwaning’inizie juu kidogo kutoka usawa wa ardhi. Hii itasaidia kupunguza uchafuzi wa maji na magonjwa yanayoenezwa kwa njia ya maji.

ZINGATIA= hakikisha kuwa maji ni safi na salama.
1.  CHAKULA.
Ni vema kutafuta vifaa vizuri kwaajili ya kuwawekea chakula. Tafuta vyombo ambavyo utaweza kuning’iniza/tundika juu kidogo kutoka chini kulingana na umri wa kuku. Hii itasadia sana kupunguza uwezekano wa kutosambaa kwa magonjwa hasa yale yanayoenezwa kupitia viatu tunvyo vaa tunapoingia bandani. Pia itasaidi sana kupunguza chakula kinacho mwagika chini wakati kuku wanapokula.
Kwa mfugaji yeyote wa kuku anapaswa kuelewa kuwa chakula cha kuku ni ghali. Hivyo ni vema kufuata taratibu vizuri katika ulishaji na kutengeneza/kununua vyombo ambavyo kuku hataweza kumwaga chakula. Kumbuka kwamba kama vyombo siyo vizuri basi vitamwaga chakula kingi na hivyo kukuletea hasara.
Ili kuweza kupata mazao mazuri yenye faida, ni vema ununue chakula cha kuku madukani au utengeneze wewe mwenyewe kama nitakavyoeleza hapa chini ili uwape kuku wako chakula chenye viini lishe vyote muhimu kwa kuzingatia umri wa kuku ulionao. Kwa vifaranga, unaweza kuwawekea chakula chini kwenye magazeti/mifuniko ya ndoo/sahani. Baada ya siku 10 unaweza kuwawekea kwenye chombo maalum.
1.       Namna ya kuandaa chakula cha kuku.
Vyakula vya kuku vinapaswa kuwa na aina/viini lishe muhimu kama vile Protini, Wanga, madini na Vitamini.
Vyakula hivyo vimegawanyika kama ifuatavyo;
o   Vyakula vya kujenga mwili ni; Jamii ya kunde,samaki, dagaa,mashudu ya ufuta/alizeti/pamba,
o   Vyakula vya kulinda mwili ili usipatwe na maradhi ni; Mafuta ya samaki na majani mabichi kama vile; kabichi, mchicha,majani ya mpapai na nyasi mbichi.
o   Vyakula vinavyojenga mwili/mifupa ni kama vile; Aina za madini, chokaa, chumvi na mifupa iliyosagwa.
o   Vyakula vilivyotajwa vinaweza kumkuza vizuri kuku hadi uuzwaji/kuliwa kwake. Surghum Larrymeal huzuia kudonoana, huboresha kiini cha yai na kuongeza mayai. Changanya kg 1 kwa kg 50 za pumba.
Ukosefu wa madini kama fosforasi na kalsiam husababisha matege, vidole kukunjamana, kufyatuka kwa misuli ya magoti, kuwa kilema na kupofuka macho kwa kuku.
Mfugaji wa kuku anaweza kununua vyakula hivi kwenye maduka ya pembejeo za kilimo/mifugo. Na kama huwezi unaweza kujitengenezea wewe mwenyewe kwa kukusanya mahitaji muhimu ya viinilishe kama ifuatavyo hapa chini;
Aina ya chakula
Kiwango cha uchanganyaji (%)
Vyakula
Vifaranga
(Kgs)
Kuku wa Nyama
(Kgs)
Kuku wa Mayai
(Kgs)
Mahindi
70
70
70
Ulezi
20
40
40
Mtama
20
30
30
Mpunga
40
70
70
Ngano
5
40
40
Pumba za Mahindi
10
20
20
Pumba za Mpunga
10
20
20
Pumba za Matama
10
20
20
Pumba za Ngano
5
15
15
Mashudu ya Nazi
10
30
40
Mashudu ya Pamba
5
10
10
Mashudu ya Alizeti
10
20
20
Mashudu ya Ufuta
10
10
5
Damu iliyokaushwa
5
5
5
Mifupa iliyosagwa
5
5
7.5
Dagaa
10
5
5
Lucina
5
5
5
Chokaa
5
5
5
Chumvi
0.5
0.5
0.5
Soya
10
20
20
Sorghum Larry Meal
1
1
1

1.       NB. Kabla ya kufanya kazi hii unaweza ukamuona mtaalam wa mifugo kwa ushauri zaidi kama utaona ni muhimu.

Mfano wa namna ya kuandaa kilo 100 za chakula cha kuku.
1.  Mfano wa chakula cha vifaranga kuanzia umri wa siku 1-wiki 4.
VYAKULA
KIASI(Kilogram) KG
Mahindi
30kg
Pumba za Mahindi
20kg
Soya
18kg
Mashudu ya Alizeti
20kg
Dagaa
5kg
Mifupa iliyosagwa
4kg
Chumvi
0.5kg
Vitamini
2.0kg
Jumla 100

1.  Mfano wa chakula cha kukuzia kuanzia Wiki 4-8
VYAKULA
KIASI(Kg)
Mahindi
45kg
Pumba za Mahindi
20kg
Mashudu ya Pamba
5.0kg
Soya
20kg
Dagaa
2.5kg
Mifupa iliyosagwa
5.0kg
Chumvi
0.5kg
Vitamini/Damu kavu
2.0kg
Jumla 100

MAGONJWA YA KUKU.
Kuku huweza kushambuliwa na magonjwa mengi ambayo mara nyingi husababisha hasara kubwa kwa mfugaji. Hasara hizo ni kama vile; gharama za matibabu, upungufu wa mayai, kudumaa kwa kuku, na vifo.

Magonjwa ya kuku yamekuwa ni tishio na hukatisha tamaa sana watu wanaofuga kuku. Magonjwa mengi husababishwa na Bakteria, Virusi, Vimelea, Minyoo, Viroboto, Chawa, Utitiri, Lishe duni au Uchafu. Lakini sauala hili limegundulika kuwa mara nyingi makosa ni ya wafugaji wenyewe kwani maranyingi hupuuzia suala la umuhimu wa kuwaona wataalam wa mifugo (ndege) na baadhi wanapobahatika kuwaona wataalam, basi hupuuzia ushauri wa wataalam hao.

Baadhi ya magonjwa hayo na njia rahisi ya kuyatibu ni kama ifuatavyo (nimejitahidi kutafsiri kidogo,lakini maneno mengine ni ya kiingereza ambayo sikupata tafsiri yake kwa urahisi);
1.       MAGONJWA YA NDEGE WANAOFUGWA MAJUMBANI
(HASA KUKU)
JINA LA ASILI
DALILI
KISABABISHO
(PRESUMPTIVE DIAGNOSIS)
DALILI KUU
(CLINICAL SIGNS)
MATIBABU RAHISI LAKINI MUHIMU NA HARAKA TENA KWA GHARAMA NAFUU
Kideri/
Mdondo (Newcastle Disease)
Kusinzia,
kuhara, kushusha mabawa chini, kukosa hamu ya kula nk
Newcastle Virus
Kuku kuharisha kinyesi cha kijani/cheupe km chokaa na njano, kukohoa, kuhema kwa shida, kutokwa na mate mdomoni,kizunguzungu, kishiwa na maji, kukosa hamu ya kula,kushusha mabawa chini,kuku kufa hadi 90%.
1.                                        Pilipili kichaa na majivu
2.                                        Katani/Alovera
3.                                        Kitaalam tumia chanjo ya NEWCASTLE.
4.                                        Usafi wa banda &vyombo vote.
5.                                        Usafi wa mazingira na kuchoma moto mizoga yote.
6.                                        Usiruhusu watu kiungia ovyo bandani/usiingize kuku asiyechanjwa.
7.                                        Fuata ushauri wa daktari          



 


Ndui (Fowl Pox)
Vipele kwenye upanga (Nodules) na sehemu zisizo na manyoya.
Fowl pox
Vipele kwenye upanga,masikio.miguu na sehemu zisizo na manyoya.Kuku hufa hasa wale wadogo.
o                                         Kuku wapewe chanjo, vitamin na antibayotiki (kiua vijasumu).
o                                         Uasfi wa banda na mazingira viimarishwe.
Mafua ya kuku/ Kuvimba macho
Swollen eyes/ Flu
Bakteria
Kuvimba uso na macho,kamasi hutiririka kutoka puani na mdomoni,hukohoa,huhema kwa shida na kukoroma, utando mweupe/njano kwenye macho),upofu,nk
Boresha Usafi wa banda na mazingira yake, kuku wagonjwa watengwe na ikibidi wachinjwe.
Muone mtaalam wa mifugo ili upate chanjo.
Ugonjwa unaoshambulia mfumo wa hewa.
Chronic Respiratory infection.
Infections bronchitis laringotracheitis/Chicken Influenza (Bakteria)
Kuku hupata Mafua, kushindwa kupumua,hutokwa na makamasi,vifaranga hudumaa,utagaji hupungua na viungo vya mifupa huvimba.
Boresha usafi, hakikisha kuna hewa ya kutosha.
Muone mtaalam akupe antibayotiki huponya/kwa ushauri zaidiTenganisha kuku wenye ugonjwa.
Gumboro/Kuhara chokaa
Whitish diarrhoea
Fowl typhoid
Vifaranga kuharisha kinyesi cheupe, kupungua uzito,hushindwa kuhema,manyoya husimama,hutetemeka na hatimaye hufa.
Chanja vifaranga wakiwa na umri wa siku 1.
Zingatia usafi wa banda, vyombo vya maji na chakula.
Tumia mkaa.
Hakuna tiba ya kitaalam
Viroboto/ Utitiri/
Fleas/mites
Ectoparasites
Fleas around the eyes, Restlessness (Kutulia kwa muda mrefu bila kuchangamka)
Tumia kuweka majivu bandani. Kitaalam tumia dawa yenye unga kama poda.
Papasi
Soft ticks
Soft ticks
Sores on skin(Vidonda kwenye ngozi), Paralysis(ku, Anaemia
Tumia kuweka majivu bandani. Kitaalam tumia dawa yenye unga kama poda.
kunyonyoka manyoya

Minyoo/bacteria
Kunyonyoka manyoya na kubaki mtupu. Shingo kurudi nyuma, kushindwa kula vizuri.
Tumia kinysi cha n’ombe. Kitaalam tumia Vitamin B12 na Egg Plus Fomula.
Kuhara choo cheupe
White Bacillary Diarrhoe

Zaidi ni kwa vifaranga kabla ya wiki 4 kuhara mharo mweupe.
Tumia mkaa, Alovera.
Kitaalam tumia OTC+
Homa ya matumbo
Bloody diarrhea/
Typhoid
Coccidiosis
Ugonjwa huu huambukizwa kupitia maji/mayai/kinyesi/kudonoana na mazingira machafu. Kuku huharisha mharo wa kijani, vilemba na upanga hupauka kutokana na upungufu wa damu,manyoya kusimama.
Tumia mkaa, Alovera.
Vitunguu swaumu robo kilo ikitolewa maganda,ikatwangwa na kuchanganywa na maji lita 1,chuja na kuwapa maji yake kwa wiki 1.
Ondoa kuku wenye ugonjwa na usitumie mayai yenye ugonjwa kuanguliwa vifaranga.
Kitaalam tumia Furazolidone.
Muone mtaalam
Kuvimba miguu
Swollen legs
Scaly legs
Scales on legs(mikato miguuni), lameness.
Tumia Alovera
Muone mtaalam
Kipindupindu cha kuku
Fowl Cholera
Bacteria
Mharo wa njano, husinzia na kulegea,hulala kichwa kikining’inia kwenye mabawa,manyoya husimama,hushindwa kuhema na hatimaye hufa.
Imarisha usafi wa banda,vyombo na mazingira yake.
Kitaalam unaweza kutumia dawa aina ya Salfa/muone daktari.
Mayai kuvunjika tumboni
Broken eggs in abdomen
Egg peritonitis
Sleepy, on PM broken eggs with foul smell
Muone mtaalam kwa ushauri.
1.       Kwa kutumia dawa za asili nilizosema hapo juu;
1.  Pilipili kichaa 50, twanga, changanya na majivu kikombe cha chai 1, weka maji Lita 1 wape kuku.
2.  Katani/alovera. Ipondeponde, iloweke kwenye maji usiku kucha, wape wanywe.
3.  Mkaa. Kama kuku wako wanaharisha,Chukua kiasi cha mkaa, kitwange, changanya kwenye chakula, wape, hawataharisha tena. Mama E.G.White katika kitabu chake cha Uponyaji wa Mungu Uk.64 ameeleza juu ya Tiba ya Mkaa. Jaribu uone mafanikio yake kwa kuku anyeharisha kawaida na siyo kideri.
4.  Kinyesi cha Ng’ombe. Kausha kinyesi cha ng’ombe, kisage na kisha changanya na chakula cha kuku. Hii inasaidia sana kwa kuku wanaonyonyoka manyoya.

1.       MINYOO.
Hawa ni wadudu wanaoleta madhara kwa kuku na wanyama wengine pia. Kuku hupata minyoo kwa kula vyakula vyenye wadudu/vimelea vya wadudu hao.

Dalili. Kuku Hudumaa, manyoya huwa hafifu, hupungua damu na uzito, utagaji wa mayai hupungua, minyoo huweza kuonekana kwenye kinyesi.

Namna ya kuzuia minyoo.
o   Safisha banda mara kwa mara (ukiweza tumia dawa za kuua wadudu)
o   Badilisha matandazo mara kwa mara.
o   Safisha vyombo vya chakula na maji mara 2/3 kwa siku.
o   Tenganisha kuku wakubwa na wadogo.
o   Wape kuku dawa za kuzuia minyoo kila baada ya miezi 3.
o   Muone mtaalam kwa ushauri zaidi.

1.       MAGONJWA YANAYOWEZA KUSABABISHWA NA UPUNGUFU WA CHAKULA/VIINI LISHE.
Iwapo kuku watapewa chakula chenye viini lishe kidogo/kisicho na viini lishe muhimu kama vile; Protini, Wanga, Madini na Vitamini wanaweza kupata madhara yafuatayo;
o   Kudumaa,
o   Kupungua uzito,
o   Kupungukiwa na damu,
o   Mifupa kupinda/kuvimba/kutokuwa imara,
o   Utagaji wa mayai hupungua na uangaji wake pia huwa hafifu,
o   Ganda la yai huwa laini,
o   Manyoya huwa machache na laini,
o   Kujikunja kwa shingo/miguu na vidole,
o   Kuwa na majimengi mazito chini ya ngozi ya kifuani,
o   Kupata magonjwa mara kwa mara,
o   Hali hii inaweza kusababisha Kuku kufa.
2.       Namna ya kuzuia.
o        Kuku wapewe chakula chenye mchanganyiko wa viinilishe vyote muhimu kama vile Vitamini, madini na Chokaa kufuatana na umri/aina na mahitaji yake.
o        Wapewe majani mabichi kama mchicha, kabichi na majani ya mapapai.
o        Wapewe mchanganyiko wa vitamin na madini kama chokaa na chumvi kwa kiwango maalum maana ikizidi pia yaweza kuathiri kuku.
3.       MUHIMU.
Ili liziua magonjwa ya kuku na kupata faida kubwa kwa kufuga kuku, ni muhimu sana mtu anayehudumia kuku bandani aweze kutambua haraka dalili za magonjwa ya kuku kama nilivyoeleza hapo juu ikiwa ni pamoja na kuzingatia usafi wa banda. Ni lazima ajue tabia ya kuku ya kila siku. Kuku mgonjwa unaweza kumtambua kwa kuangalia yafuatayo;
o        Tabia ya kuku.
o        Kinyesi cha kuku (mabadiliko ya kinyesi).
o        Ulaji wa chakula na unywaji wa maji kama umepungua.
o        Utagaji wa mayai na uimara wa mayai kama vimepungua.
o        Kuku kutochangamka.
o        Vifo ni dalili ya mwisho.

Kama utaona kuna kuku mgonjwa bandani basi mtenge na wenzie kama unavyowafanyia vifaranga. Ili uweze kuwahudumia peke yao. Wengine ambao hawajaonesha dalili wapewe dawa ya kinga haraka iwezekanavyo kupitia ushauri wa mtaalam wa mifugo aliye karibu.

Chanjo na matibabu yoyote yafuate ushauri wa mtaalam/mtengenezaji wa dawa husika bila kupuuzia ili upate mafanikio. Hii itakuwezesha kupunguza/kuponya magonjwa na kupunguza gharama za matibabu na vifo. Hakikisha kuwa chanjo/tiba zinatoka kwa mtaalam anayejua kutunza chanjo/dawa kwenye ubaridi unaotakiwa kulingana na maagizo ya mtengenezaji.
1.       ANGALIZO
Mambo yafuatayo yanaweza kusababisha magonjwa au kupunguza uzalishaji hivyo kuleta hasara zisizo za lazima kwa mfugaji.;
1.  Kufuga kuku wengi kwenye eneo dogo.
2.  Chumba/banda lisilo na hewa na mwanga wa kutosha.
3.  Banda kuwa chafu.
4.  Vyombo vichache/visivyotesheleza kwaajili ya chakula na maji.
5.  Vyombo vichafu vya maji na chakula.
6.  Chakula kisicho na viini lishe vya kutosha/kichache.
7.  Kubadili ladha ya chakula.
8.  Kuchelewa kudhibiti magonjwa ya kuku.
9.  Kuchanja/kutibu kuku bila utaratibu/ushauri wa kitaalam.
10.    Kutishia kuku wakati wa kuingia bandani/kuwashika/kuwasumbuasumbua.
11.    Mabadiliko ya hali ya hewa.
12.    Kufuga kiholela bila kuwachambua.

1.       MWISHO
o   Chagua njia bora na rahisi inayokufaa kulingana na eneo ulilopo na mahitaji yako pia. Angalia njia itakayokupa faida kwa gharama ndogo.
o   Chagua kuku wenye uwezo wa kukua haraka, wanaostahimili magonjwa, wanaotaga mayai mengi, wanaoweza kuangua vifaranga wengi na kuwalea.
o   Chagua jogoo aliye na uzito mzuri na mwenye kucha fupi.
o   Uwiano wa jogoo kwa majike iwe ni jogoo 1 kwa majike/mitetea 10.
o   Kuku anayetazamiwa kuatamia mayai anatakiwa asiwe na chawa/viroboto/utitiri.
o   Kuku ambaye hakidhi sifa za kuwa kuku bora anayefaa kuwa kwenye kundi inafaa aondolewe ili asilishwe kwa hasara awapo bandani.
Waafrika tulio wengi hatuna utamaduni wa kutunza kumbukumbu. Ni vizuri basi uanze kutunza kumbukumbu za mwenendo wa kazi zako za ufugaji wa kuku. Hii itakurahishia sana kujua faida, hasara na hata kujua namna bora ya kuboresha ufugaji wako. Kwa mfano;
7.  Kumbukumbu za uzalishaji mayai zitakuwezesha kujua kiasi cha mayai yanayotagwa kwa siku. Idadi ikiwa chini ya 60% utagaji huo siyo mzuri hivyo utatafuta sababu ya tatizo nk. Utagaji unatakiwa uwe 70% hadi 95%.

1.  Kumbukumbu ya vifo itakusaidia kujua hatari itakayokujia. Mfano vifo vikizidi 1% inaashiria tatizo la ugonjwa. Hivyo uchunguzi ni lazima ufanyike ili kutatua tatizo.
2.  Kumbukumbu za mapato na matumizi pia zitakusaidia kujua faida na hasara nk. Hapa utajua ni ghara kiasi gani ulitumia kufuga na faida kiasi gani umepata baada ya mauzo ya mayai/kuku husika.
Hii ni mifano.
1.  MAYAI YALIYOTAGWA KWA SIKU.
TAREHE
Kiasi cha Mayai yaliyotagwa
Asubuhi
Jioni
Maoni









Jumla



2.  KINGA NA TIBA ZA MAGONJWA YA KUKU
TAREHE
UGONJWA
GHARAMA



Shs
Maoni




Jumla





1.  MATUMIZI YA CHAKULA KWA MWEZI
TAREHE
AINA YA CHAKULA
KIASI (KGS)
GHARAMA



Shs




Jumla




1.  KUMBUKUMBU YA MAUZO YA MAYAI/KUKU
TAREHE
IDADI YA KUKU WALIOUZWA
MAPATO
MAJIKE
MAJOGOO
MAYAI
Shs











Jumla





1.  KUMBUKUMBU YA MAPATO NA MATUMIZI.
MAPATO
MATUMIZI
TAREHE
MAUZO
SHS
TAREHE
MANUNUZI
SHS












JUMLA


JUMLA



1.       FORMULA 100Kgs za Chakula cha Kuku
1.  Mahindi yaliyoparazwa 25Kgs.
2.  Pumba za Mahindi 25Kgs.
3.  Dagaa/Uduvi 10Kgs.
4.  Unga wa Mifupa/Bionemeal 5Kgs.
5.  Chokaa/Limestone 5Kgs.
6.  Mashudu ya Alizeti 5kgs.
7.  Mashudu ya Pamba 10kgs.
8.  Ngando ndogondogo 5kgs.
9.  Machicha ya ngano/Wheat Brand 10kgs.