Monday, March 19, 2012

AFYA YA UZAZI

Afya ya Uzazi Upangaji familia na Ulezi
Wanawake wengi hujiuliza “Na je, kama nina mimba?” wakati mwingine maishani. Kama unajiuliza kama una mimba una maswali mengine Chunguza Beehive’s pregnancy & parenting kupata ujumbe zaidi kuhusu upangaji familia, jinsi ya kujua kama una mimba na chaguzi ulionazo kama una mimba.Unaweza pia kujua kuhusu fungu lawamu za mimba, umuhimu wa utunzi wa mzazi wa mapema, unachofaa kufanya wakati wa kujifungua na jinsi ya kulea mtoto awe na afya nzuri.

Kumtunza mtoto wako
Ni jambo la busara kujitunza wewe na mwanao. Kutunza mtoto wako linaweza kuwa jambo la kukufurahisha, lakini ni kazi ngumu. Utampatia mtoto chakula/utamlisha mtoto mara ngapi na baada au wakati gani? Wewe hufanya nini mwanao anapolia au anapougua? Unozuiaje maradhia?

Unaweza kuwa mwepesi kushtuka/utakuwa na wasiwasi au lakini utayagundua hayo haraka. Utashtuliwa na ambayo unajua tayari. Katika sehemu hii, utapata kujua unayofaa kufanya utakapomleta mwanao nyumbani

Kumpeleka mwanao nyumbani
Mtoto aliyezaliwa anajiratibisha na ulimwengu ulio tofauti na joto na usalama wa tumbo la mamake. Watoto hawa wanastahili kupendwa,kulishwa, kuwekwa safi na wakiwa na joto inayofaa. Kuna mambo mengi mapya wazazi wanapaswa kujua.

Afya ya mwanao
Unafaa kumwita/kumpigia daktari wako kama utaona uafuatayo kwa mwanao:

Kukosa kula/kukataa chakula
Kuwa na rangi isiyostahili
Nguvu kidogo
Joto la juu ya 380c chini ya kwapa
Ghasia/fujo zisio za kawaida
Kulala zaidi ya kawaida
Kutapika au kuhara
Shida za kupumua

No comments:

Post a Comment